Tags:
Replies are closed for this discussion.
Sasa kaka Don je wewe ni mukulima; na unalima nini sana sana........................
1.Jina la Don limetokea wapi? Au jina lako halisi? Kama siyo,kwa nini umependa kutumia jina la bandia badala ya kutumia jina lako halisi?
2.Unajishughulisha na nini huko Mamtoni?
3.NIni kilikufanya uondoke nchini kwako (TZ) na kwenda kuishi huko ulipo?
Hongera kaka Don!
Lutamyo sielewei kama unaliza swali au maswali maana hakuna alama ya kuuliza!! anyway ngoja nifanye kuwa ni maswali.
Mimi ni mkulima ikizingatiwa nimezaliwa katika family ya wakulima, na ninalima mbogamboga
Lutamyo J. Kingdom said:
Sasa kaka Don je wewe ni mukulima; na unalima nini sana sana........................
1.Severini jina la Don(sio jina langu halisi) chimbuko lake ni katika kijiji cha Fotobaraza, kule nilikuwa Promota wa CHAOGA na PASCAL katika mashindano ya kubugia Ulabu(Bia) hivyo wanakijiji wakanipachika jina la Don.Kwakuwa waanzilishi wengi wa kijiji hiki tulitoka kule Fotobaraza hivyo niliona vema niendeleze jina walilonipa.
2.Huku mamtoni najishughulisha na kubeba BOX
3.Hakuna kingine zaidi ya kutafuta good life
Severin said:
1.Jina la Don limetokea wapi? Au jina lako halisi? Kama siyo,kwa nini umependa kutumia jina la bandia badala ya kutumia jina lako halisi?
2.Unajishughulisha na nini huko Mamtoni?
3.NIni kilikufanya uondoke nchini kwako (TZ) na kwenda kuishi huko ulipo?
mkuu alex magere aka DON KING, hongera kwa kuwa mdau wa wiki.
Hongera sana mkuu Don.
je unaonaje misha ya kubeba box ukiwa mamtoni na ukiwa tz?
na ukiangalia ugumu wa maisha umekuwa ukibana kotekote naweza kusema huko mamtoni ndio zaid kulingana na maisha yalivyo na bei za v2 watu wake cc huku ukikosa unaweza kumpiga kirungu Mr Tulonge akakupa buku maisha yakasonga but huko huwezi tembeza virungu je nafikiri unaweza kupata maisha bora kwa kubeba box?
unafikiri kwa hapa tz bila kukimbilia mamtoni vijana tufanyeje? ili tuwe na maisha mazuri? maana ajira za tz kama unavyozijuwa mshahara haufiki tarehe 7 umeisha kisha unaanza tena kukopa na tunatamani maisha bora tutayatowa wapi?
1. Umeoa au unaishi na msichana bila kumuoa? Maana huwa naona picha zako tu,za mwenzi wako sizioni.
2. Una watoto wangapi? Wa nje au ndani ya ndoa?
3. Unalizungumziaje suala la kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa?
4. Unampango wa kupata watoto wangapi?
© 2023 Created by Tulonge.
Powered by