Tulonge

Mwanamke akitoka nje ya ndoa huonekana malaya saaaana mbele ya jamii,ila mwanaume ni kawaida tu.

Inanikera sana,Imekuwa ni kitu cha kawaida sana kwa wanawake kuonekana malaya sana pale inapogundulika ametembea na mwanaume mwingine nje ya ndoa yake,hata kama ni mara moja tu. Lkn mwanaume akitoka nje ya ndoa hata mara 100 huonekana ni kitu cha kawaida tu,na hujiona wana haki ya kufanya hivyo. Hata jamii haiwezi mchukulia vibaya sana ukilinganisha na mwanamke akifanya hivyo.

Unaweza mfumania mumeo zaidi ya mara 10 lkn yakaisha juu kwa juu hata kama ukilifikisha suala hilo kwa wazazi wa pande zonde mbili.Lkn akifumaniwa mwanamke siku 1 tu huwa ni balaa,utasemwa na familia za pande zote mbili na majirani pia autadhani umeua mtu. Pia taraka itakufuata nyuma.

Hii ni haki?

Views: 1841

Reply to This

Replies to This Discussion

Si kwamba natetea upande mmoja tu,ila inawezekana ikawa haki kwa sababu,kwa mwanaume si jambo la kunyoshewa kidole anapochukua uamuzi wa kumiliki mwanamke zaidi ya mmoja ndani ya nyumba moja.Je,ulishawai kuona wapi mwanamke ana mwanaume zaidi ya mmoja ndani ya nyumba moja? Vivyo ivyo haitokuja tokea ndani ya jamii mwanamke akawa treated sawa na mwanaume anapobainika kwa kufumaniwa! Hata ivo dada zanguni,globalisation isitudanganye hata kidogo kwa kauli mbiu ya gender balance,mwanaume na mwanamke haiwezekani hata kidogo wakawa sawa kihaki,ilisha kuwa proved tangu enzi za uumbaji,tusiipinge nature jamaani  kwa kuzilinganisha izi jinsia mbili,japo kila jinsia ina umuhimu wake kwa kila wakati na mahali inapobidi kuwa ivyo! Ila si kwa sababu iyo kwamba wanaume tuvimbe vichwa kwa nafasi tuliyopewa kufanya mambo yasiyo ya msingi!

Pole mrembo!!!

hiyo ndio jamii tunayoishi......

yenyewe huwa inajiona iko sawa isipokuwa mwanajamii ndio mkosefu!

Kaka edwin ulishajibu vya kutosha tuko pamoja, sina maelezo mengi hapo,,,,
Kumbe na wewe Diana umeliona hilo,yani wanajiona wenyewe wana haki kweliii.Tena wenzetu ndo wameamua kumpa haki ya kuwa na wanawake wanne,ila mwanamke haruhusiwi kuwa na mume zaidi ya mmoja. Uonevu huo
Hakuna mwanamke awezae kutumikia mabwana wawili
Jamani wadau jambo hili ni la kimaadili zaidi, kwa mtu mwenye kuelewa nini maana ya maadili kumsaliti mwenzie lazima ajiulize mara mbili. Lakini ikitokea lawama zote asitupiwe mwanamke kwa maana inawezekana mwanaume mwenyewe kasababisha, hamtimizii dada wa watu yale yanayotakiwa.

ok inanilazimu nielezee vizuri kidogo, kifupi ni hivi, kwanza ninavyofahamu mimi, kutokana na mazingira tuliojijengea zaidi, huwa mwanamke akiwa mzinzi huwa tunamuina malaya, mwanaume huwa tunamuita muhuni, kwahiyo, kuna tofauti hapo,

halafu mada ya mwanamke kutoka nje ya ndoa na kuitwa malaya kunasababu nyingi zinazoongelewa kwamba hatoshelezwi na mumewe, kumbe tulisha sahau, kwamba binadamu wote hatufanani kitabia, wapo wanawake hurka yao ni hiyo, kwamba yeye hata atoshelezwe vipi atatoka tu nje ya ndoa, wapo wasiotoshelezwa na akajua huyu ni mumewangu nifanye nini ili anitosheleze, nicheze nae vipi ili namimi nisijitie aibu kwenye jamii nikamzalilisha mumewangu au na mimi wakaniona malaya,

na kwa upande wa wanaume, nao kama nilivyoeleza hapo juu,

 

kwahiyo jibu ni kwamba, kukitoka nje ya ndoa kama ni mwanamke kama jamii itakuona lazima wakuite malaya, na kama ni mwanaume lazima wakuite muhuni, mzinzi, msaliti wa ndoa yako, wewe jitulize na mpenzi wako au mume wako mmoja uone kama watakuita hivyo,

binadamu huishi kulingana na mazingira aliojengewa tangu awali,,,

 

                                                      TAKE CARE UKIMWI UPO NA UNAUA,,

                                                       SASA HIVI KULIKO MALARIA

Hapa natoa macho tu na misikio kusikiliza wadau mnavyolonga. Ngoja nimalize kusoma habari ya uzinzi wa Arnold Schwarzenegger na pia yule boss wa IMF aliyetiwa ndani huko New York kwa tamaa ya ngono (uzinzi) halafu nitarudi baadae ku-comment. 

 

Hahahhahaaaa Dada Diana naona umeguswa sana na hii ishu. Naona na wewe unakomaa ili upate haki yako ya kutoka nje bila kunyooshewa vidole na wanajamii kama mwanaume.Kweli wanawake mmeshupaa kudai usawa kwa sasa.
It is said that men are polygamous by nature so they are polygenry and now days women have become polygandry which has become a normal thing. But, a lady to have two or more men it awkward. Anyway "what a man can do a woman can do it better"

Diana mpenzi !

Nasema kauli ya jibu lake - NDIO NDIO KABISA !!!

MWANAMKE kwenye ndoa hapaswi kabisa kutoka nje ya ndoa yake,kufanya hivyo ni UMALAYA ,LAANA na kila aina ya matusi anastahili kupata.

Haya yanajiri kwasababu 2 nzito ambazo kwakwe ni kufuli:

  1. Yeye ni mmilikiwa wa ndoa hutolewa mahari na kupewa matunzo ya gharama zake zote za kimaisha ambazo ni haki zake kisheria.
  2. Yeye ndie anaebeba mimba na kuzaa watoto wa familia mahsusi.

Kitendo chake cha kutoka nje ya ndoa ni dhulma na uhaini,kwani kutembea na mwanamme mwengine asiekuwa mume kuna haya yana nafasi ya kutokea :

  1. Kuchukua mimba ya nje akaweka ndani ya ndoa.
  2. Kuweza kurubuniwa kwa zawadi akashawishika hata kufanya kinyume cha maumbile
  3. Uzoefu wa uchafu wa nje utapelekea kuharibu fikra kisaikolojia na kuja na madai ambayo hayapo awali.
  4. Kutembea kwakwe nje,kunaondosha uaminifu ya kulinda hadhi na mali ya familia yake.
  5. Kunamuandalia chuki miongoni mwa ukoo wa familia ya mume na washirika wa bwana huyo- n.k

Wito kwa wanawake wenye ndoa waheshimu mipaka yao.

Na huyu mwanamme anaetembea ovyo nje ya ndoa yake ana haya yafutayo:

  1. Anapoteza nguvu na kutupa watoto nje wasio hatia.
  2. Anajikumbia hatari za gonjwa au magonjwa ya zinaa
  3. Anajiongezea gharama zisizomlinda na mwisho wake ni ufukara- N.K

Wito kwa wanaumme wenye ndoa ni vyema waheshimu ndoa zao.

Lakini majina mabaya hayamfiki mwanamme kwa vile yeye kwa yeye ajipotezea binafsi yake lakini mwanammke anavuruga na kuandaa hatari ya jamii yote inayomzunguka.

Ndio,(Allah S.W) AKATUHALALISHIA wanaumme kuoa zaidi ya mke mmoja kwa kuweka msingi imara wa ustawi wa jamii miongoni mwa watu na maisha yao.

DIANA ! mwanammke kuwa MALAYA - NOOOMAA!  mwanamme -NOOMA KICHIZI

Huo ni mchango wangu kwa wanatulonge !!!!

 

Reply to Discussion

RSS

© 2023   Created by Tulonge.   Powered by

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

/* \uascript type="text/javascript">\udinsert below header image\udif (typeof(x$) != 'undefined') {\ud var postHeaderImageAd = '\uadiv id="postHeaderImageAd ">\ua\ua/div>';\ud x$("#xg_masthead").after(postHeaderImageAd);\ud}\ud \uascript type="text/javascript">\ud insert below header image \udif (typeof(x$) != 'undefined') {\ud var postHeaderImageAd = '\uadiv id="postHeaderImageAd ">\ua\ua/div>';\ud x$("#xg_masthead").after(postHeaderImageAd);\ud}\ud /*