Tulonge

 

Wengi wetu tumezoea kula vyakula tulivokula kwa mazoea tunamoishi. Unaenda ugenini au nchi ya ugenini, siku ya siku wakutana na wenyeji na wanakukaribisha nyumbani kwao kwa chakula mchana au jioni. Baada ya chakula kuwekwa mezani kama ilivyo pichani hapa juu unauliza hicho kwa sahani ni nini? Unaambiwa na wenyeji wako ni panya wa porini kabanikwa kwa moshi na ndio chakula cha asili cha wenyeji wako. 

 

Wana TULONGE naomba mnambie..... Je iwapo ni wewe utafanya nini? Utasema wazi chakula cha namna hiyo hujakila toka kuzaliwa hivyo hupendelei kula utabakia njaa? Au utajitahidi kula na kuwa polite kwa wenyeji wako?   

Views: 2957

Reply to This

Replies to This Discussion

Doh!ni kweli wengi wetu tumezoea kula chakula cha aina moja ambacho tumekizowea,ila ni vizuri pia kujifunza kutoka kwa wengine kama hakikudhuru,mimi hapo mbona ningekula angalau nijue tu hata test yake.mbona mzungu anaweza kula mlenda na ugali kwa mikono.

Mary umesema kweli.... mie nimejikuta nakula vyakula vingi sababu ya safari zangu. Na mara nyingi najisikia aibu kukataa kwani watu wamehangaika kupika. Panya pori wa kuchoma nimemla tena mtamu sikutegemea.

Ukienda ROMA fanya kama WAROMANI wafanyavyo!!! vinginevyo utakufa kwa njaa bure!

duh japo nitastuka kidogo lakini, nitajaribu kwani hapo sina jinsi ndiyo kwanza nipo ugenini,

Kama wao wanakula na mimi nakula tu. Kwanza wagogo wa Dodoma wanagonga sana hawa panya na hawafi wala nini.

Dismas.. sikujua wagongo wanakula hawa panya pori ila nilisikia watu wa mkoa ya Mtwara sijui Lindi wanakula panya. Panya wanaliwa nchi nyingi maana Mozambique, Malawi, Zambia na Zimbabwe wanakula panya pori.

Magere na mama Manka ni kweli, ugenini unaogopa na hasa ukiwa na njaa unakula. LOL....

umesahau ule msemo kuwa kiingicho si najisi ila kitokacho

Mmmmmmh unaweza jilazimisha ili ule 7bb wenyeji wanakula ila ukikumbuka unakula panya unaweza rudisha chenji (kutapika)

haaa mama malaika....nasikia watamu hao  kama nyama ya kuku......Ila wanaoliwa ni wale wa porini wanaojitafutia chakula wenyewe...nafanafa  na mbegumbegu

Ha haa haa haaa..... jamaa kanifurahisha aliposema "njomba hii kitu kunoga hawa". Naona wachina wakifika sehemu hii wanafurahi sana maana wao wanakula vyote hadi mbwa.

 
Gratious Kimberly said:

haaa mama malaika....nasikia watamu hao  kama nyama ya kuku......Ila wanaoliwa ni wale wa porini wanaojitafutia chakula wenyewe...nafanafa  na mbegumbegu

Mi nazan ntakufa nanjaa kwakweli. Cwez kumla ntatapika.

Reply to Discussion

RSS

© 2023   Created by Tulonge.   Powered by

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

/* \uascript type="text/javascript">\udinsert below header image\udif (typeof(x$) != 'undefined') {\ud var postHeaderImageAd = '\uadiv id="postHeaderImageAd ">\ua\ua/div>';\ud x$("#xg_masthead").after(postHeaderImageAd);\ud}\ud \uascript type="text/javascript">\ud insert below header image \udif (typeof(x$) != 'undefined') {\ud var postHeaderImageAd = '\uadiv id="postHeaderImageAd ">\ua\ua/div>';\ud x$("#xg_masthead").after(postHeaderImageAd);\ud}\ud /*