Jamaa mmoja ambaye alikuwa hajala kuku kwa muda mrefu alitoa kali ya mwaka siku moja baada ya kufanikiwa kupata kitoweo hicho ambacho kilipikwa nyumbani. Baada ya muda, mkewe alifuata maji kisimani, jamaa aliangalia kulia na kushoto akadokoa nyama na kwenda kuitafunia chooni.
Baada ya muda mkewe alirudi, alimwita mumewe lakini hakuitika akajua alitoka. Naye alichukua kipande cha nyama na kwenda nacho chooni. Ile anaingia huku mkononi ana kipande cha nyama, alikutana na mumewe naye akimalizia mfupa. Ili kuua soo huku akicheka alisema; “Mume wangu kumbe na wewe unaonja.” Hakuna wa kumsema mwenzake ngoma droo.
Tags:
Hahahahahaaaa Christer ungekuwa muwazi tu.hapa itakuwa ni wewe na Alfan.
Hahahhahahahaaaaaa, wivu unakusumbua wewe!! mi na alfan hatuna mambo hayo!
Hahahahah,hii imeniacha hoi.!kuku bwana usicheze nayo ni kitoweo cha kiakili,kikitia maguu home kidogo kunakuwepo furaha.
ha haaaa,haa haaa.wote wanaonja.
huyu ndege mtamu kwelilkweli
© 2021 Created by Tulonge.
Powered by