Mama mmoja alimshuku mume wake anatembea na house girl, siku moja mume bila kuwa na taalifa mama akampa ruhusa ya week house girl akaone wazazi wake ili amteg mumewe, usiku kabla mume hajarudi ktk mishemishe mama akajichomeka chumbani mwa yule house girl akazima taa na kujifanya amelala mara akasikia mtu anajiingiza chumbani na kumparamia, mapenzi moto moto yakaanza jamaa kumaliza 2 mama akamwambia enhee siku zote nilikuwa nakutega leo nimekukamata ile kuwasha taa ili amumbuwe mumewe akakuta ni mlinzi wao, je wewe ungefanyaje?
Tags:
Hahahhahahhaahaaaaaa mama kajiumbua mwenyewe. Alijifanya mtaalmu wa mitego hhahaahhahaaaaa.Mama imekula kwako sasa.Tena angetiwa mimba kabisa ingekuwa safi sana.
Ha haa haaa.... naona mama alifikiri mumewe kapata Anold Schwazeneger syndrome, kumlamba mtumishi wa ndani.
Aibu kubwa sana, sijui huyo mama uso wake aliufunika vipi baada ya kutoka humo chumbani? Omary, mie sijawahi kuwa na beki tatu (house girl) hivyo inakuwa vigumu sana kufikiri ningefanyaje. Ila kwa uelewa wangu ningemuingia mume wangu kiutani-utani tena taratibu kujua nini kinaendelea kabla sijaanza kuchukua uamuzi wowote.
hahahahahah safi sana Mama napenda Mama kama wewe sio huyo mather kakurupuka matokeo yake kagawa uroda kwa mlinzi sasa kajiumbuwa mwenyewe. Dis mzee wa mimba unapeeenda kuwamimba wenzio nyau wee lol.
unajuwa akili haikuwa kwenye hisia za kujuwa huyu nani? yeye alukuwa kwenye kukamata mwizi yaani mawazo yake yote yalikuwa kumuumbuwa mumewe pia unajuwa ukifanya kitu kwa wizi hakuna maandalizi yaani k2 cha fasta uondoke bi mdash akaona leo kafumania kumbe anajigawa kiulaiiin kwa Mr Tulonge lol.
Ha ha aa haa haa haa haa haa haaa ....... eti anajigawa kwa Mr Tulonge.
Omary said:
unajuwa akili haikuwa kwenye hisia za kujuwa huyu nani? yeye alukuwa kwenye kukamata mwizi yaani mawazo yake yote yalikuwa kumuumbuwa mumewe pia unajuwa ukifanya kitu kwa wizi hakuna maandalizi yaani k2 cha fasta uondoke bi mdash akaona leo kafumania kumbe anajigawa kiulaiiin kwa Mr Tulonge lol.
Omary... ujue maamuzi ya papara na haraka bila kufikiria si mazuri. Naelewa kuwa hakuna kitu kinachouma roho kama mwanamke au mwanaume kuibiwa mali (mpenzi wake) yake. Huyu mwanamke alisahau kuwa uvumilizi na subira ndio njia pekee ya busara kujua kama kweli mumewe anatembea na house girl au la. Haya mambo ya kuhisia yamevunja mahusiano mengi sana ya kimapenzi, na ndio chanzo cha matatizo ndani ya ndoa nyingi.
Hebu fikiria mume wa huyu mwanamke akisikia kuwa mkewe kalala na mlinzi wao itakuwaje??? Mwanamke atajielezaje kwa mumewe hadi amuelewe chanzo cha kulala na mlinzi wao wa nyumbani?? Hapo si ndio mwisho wa ndoa?? Mwanaume atafikiri kumbe haya ndio mambo anayofanya mke wangu na mlinzi... hatomuamini kamwe hata mkewe alie machozi ya damu kujieleza kisanga chenyewe. Mkewe hatojitia aibu yeye peke bali atatia aibu familia nzima (watoto wake, mumewe na ndugu zake mwanamke)
Nikweli Mama uyasemayo ila wanawake wengi hawapo hivyo huwawanakurupuka tu wakisikia kitu au wakihisi kitu
wanakurupuka hawawazi kabla ya kutenda Mama wewe nikatika kundi la wanawake kidogo sana wanaojiuliza kabla kufanya au wenye maamuzi yaliotulia hongera kwa hilo mama but wengine wapaswa kujifunza kwa hili lililotokea kwa mwanamke mwenziwao.
Mmmmh ni mgeni napita tu, ila km alivyosema Holiness, mi mtu wangu namjua, hata kwenye giza totoro!!!!!! huyo mama nae bwege tena bwege haswaaaaaaa, kaniuzi mie!!
Hahahaaaa... Natamani mimi ningekuwa huyo mlizi.. kinachoonekana hapa .. huyo mlinzi alikuwa na mahusiano na huyo beki tatu.. sasa alivyoona beki tatu anasepa likizo akaona akamuage.. kumbe... teh teh teh.. kagonga mama mwenye nyumba... ha ha ha ha aaaa
HAHAAAAA!! WIVU MBAYA NA PIA KUKURUPUKA NAKO KUNASABABISHA MENGI, SASA AIBU YOTE HII HUYU MAMA ATAIWEKA WAPI SURA YAKE? HALAFU MWANAUME KAMA ANAUHUSIANO NA BEKI TATU UTAMJUA TU HUNA HAJA YA KUWA NA DARUBINI, WENGINE HUWA WA KALI SANA KWA MABEKI TATU PINDI WAWAPO NA WAKE ZAO, WENGINE HUZIDISHA MAZOWEA YAANI BADALA AKIFIKA NYUMBANI AMUULIZIE MKE WAKE ANAMUULIZIA BEKI TATU, WENGINE BILA HATA HAYA HUANZA KUTANIANA NAO MBELE YA WAKE ZAO NA KUCHEKEANA HOVYO.YAANI KAMA NI MUELEWA UTAJUA TU.
© 2023 Created by Tulonge.
Powered by