Mimi kama mimi kwa mtazamo wangu naona mapenzi ya siri yana ukomo wake marafiki zangu.Unapokuwa unapenda mapenzi ya siri sana, unampa wakati mgumu mwenzako. Ni rahisi kufikiria kwamba, unafanya hivyo kwa kuwa ama hujiamini au una mtu mwingine. Weka mambo hadharani. Mtambulishe mwenzi wako kwa marafiki zako. Jiamini, unapokutana na mtu uliyesoma naye zamani au kuishi naye sehemu moja, mwambie kwamba uliyenaye ni mwenzako na unatarajia kuingia naye kwenye ndoa. Kufichaficha kunaondoa utamu wa mapenzi. Kunazidisha maswali ambayo hayana majibu. Kama yapo ni huyo mwenzako kujijibu mwenyewe. Kwa kawaida, hatajipa majibu mazuri. Yatakuwa ya kinyume – yenye tafsiri mbaya. Kwamba yawezekana hutaki kumtambulisha kwa kuwa una mtu mwingine. Je, ni kweli? Kama ndivyo huna sababu ya kumpotezea muda mwenzako. Kama si kweli, basi amka. Gundua kwamba ulikuwa unafanya makosa na uanze ukurasa mpya.
Ni mtazamo tuu,hata wewe waweza kuwa na mtazamo wako.
Tags:
Hahahahah@Christer safi sana umempa boonge la jibu najua hatauliza tena...
Hiyo ndo dawa ya mgonjwa wa wivu alfan, full dozi. lazima apone, mi ndo doctor bwana!!
Ndio maana nakupendaga sana...lol
Christer Christopher said:
Hiyo ndo dawa ya mgonjwa wa wivu alfan, full dozi. lazima apone, mi ndo doctor bwana!!
© 2022 Created by Tulonge.
Powered by