Dhamana ya msanii wa filamu Lulu inaendelea kusikilizwa katika mahakama kuu kanda ya Dar es salaam na mpaka sasa upande wa serikali mawakili wamesema hawana pingamizi na dhamana hiyo,
Habari zilizotufikia hivi punde zinadai kuwa Mahakama kuu ya Tanzania imemwachia kwa dhamana msanii wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael aka Lulu aliyekuwa mahabusu katika gereza la Segerea jijini Dar es Salaam.
Wiki iliyopita mawakili wa muigizaji huyo waliwasilisha maombi ya dhamana kwa mahakama hiyo kuu ya Tanzania.
Wanasheria hao Peter Kibatala, Kennedy Fungamtama na Fulgence Massawe waliomba dhamana hiyo itolewe haraka kwakuwa muombaji amekaa mahabusu kwa zaidi ya miezi saba na kwamba kosa lake linaweza kupewa dhamana.
Lulu anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia Steven Kanumba April 7, 2012, huko Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.Kanumba alidaiwa kuwa kwenye ugomvi na Lulu aliyekuwa mpenzi wake nyumbani kwake Sinza. source mpekuzi.
Chanzo: audifacejackson.blogspot.com
Add a Comment
HAYA LULU NAOMBA CHUKUA NO YANGU YA CM HII HAPO NAOMBA NIGIENIJEKUKUPA POLE +255717550088
Nimepata taarifa bado hajaruhusiwa kuondoka hadi sasa.Kuna documents za Lulu zinatakiwa kuwasilishwa mahakamani kabla ya kutoka.Anatakiwa apeleke VISA nk,pia hata ruhusiwa kutoka nje ya Dar pa1 na masharti mengine kibao.Ila Dk. Chani amesema masharti yote wanaweza kuyatimiza.
sijui atatuliaaa!
Saaaaaaaaaaaaaaaafi! Lulu umetengeneza siku yangu, mungu akuongoze kwa kweli.
© 2023 Created by Tulonge.
Powered by
You need to be a member of Tulonge to add comments!
Join Tulonge