Katika siku za hizi karibuni katika kanisa flan .. kulikuwa na mchango kwa ajili ya kujenga kituo cha watoto yatima kitakacho milikiwa na kanisa hilo.. Baada ya mtoa mada ndipo vikapu vikaanza kutembezwa na kila muumini alitoa kile alichokuwa nacho huku wimbo wa "toa ndugu toa ngudu, ulichonacho wewe.. bwana anakuona mpaka moyoni mwako" ukiwa unatumbuiza.
Baadaa ya kumaliza shughuli hiyo.. pesa ikaesabiwa na kutangazwa kuwa zimepatikana shilingi laki mbili na elfu tatu..
Ghafla jamaa watatu wakaingia kanisani na bunduki mkononi, wakatoa amri .. wote chini!! Wakachukua vikapu na kunaza kupiga sachi kwa kila muumini..
Walipo maliza, wakapiga hesabu kina na kumkabidhi mchungaji kiasi cha shilingi milioni kumi na nane.. kisha na kuondoka.
kati ya waumini na hao majambazi nani aliye changia zaidi?
Tags:
Kazi kweli kweli....!!!! Na pia kati ya hao Waumini na huyo Jambazi nani ataingia katika ufalme wa Mbingu?
Hilo swali hata sipati jibu lake.. tehehee
Hahahhaahhahaaa ndiyo uamini kuwa waumini huwa wanabania pesa nyingine mfukoni badala ya kutoa sadaka zote. Hapo majambazi yatapata baraka zaidi.
tatizo hapa ni HIARI na NGUVU
watako ona pepo ni waumini kwakua walitoa kwa hiyari.
Unatakiwa utoe kwa moyo,yaani kwa hiyari yako,
sasa majambazi waliwalazimisha waumini,mimi nadhani hilo si sawa.
mkuu dick, unanikumbusha history ya jambazi liliingia msikitini na bunduki yake, akawaambia waumini anaempenda mwenyezi mungu na mtume wabaki na wasiompenda watoke nje, waumeni wengine wakatoka nje, ndani wakabaki imam na wazee wawili tu, jambazi likamgeukia imam likamwambia shehe sasa unaweza kuendelea na swala yako, nilitaka kukuondolea wanafki,
hahahahah hapa bana majambazi yatatinga motoni kwani sadaka unatakiwa kutoa fungu la 10 sasa wao wameteka zoote hawajawabakishia so kanisa limechukuwa pesa si zake ila kwakuwa zilichanganywa hazijulikani zanani ni zipi?! kanisa litakuwa halina dhambi hapo tumuachie MUNGU ahukumu maana majambazi nao wamefanya lamaana lol.
© 2022 Created by Tulonge.
Powered by